Breaking News
recent

Mafanikio yamfanya Shaa kuongeza mkataba

Mwanadada Saraha Kaisi aka Shaa anayetamba na ngoma yake ‘Sugua Gaga’ni ngoma iliyompa chati kubwa kwa mashabiki wake wa ndani na nje ya Bongo.


Shaa baada ya kuona amepata mafanikio makubwa kutokana na ngoma yake hiyo ikambidi aongeze mkataba wa mwaka mmoja baada ya mkataba wa miezi sita kuisha na Mkurugenzi wa TMK Family na Mkubwa na Wanawe Said Fella.
Mwanadada huyo alizungumza kupitia swali lililoulizwa na host wa kipindi cha Clouds E Shadee nakusema “Nimeongeza mkataba na Mkubwa Na Wanae ambao awali ulikuwa wa miezi sita sasa nimeongeza miezi sita tena na umekuwa mkataba wa mwaka mmoja baada ya kugundua kuwa ngoma ya Sugua Gaga niliyoifanya imeshika chati sana, ata hivyo natarajia kufanya ngoma kali zaidi ya Sugua Gaga.” alisema Shaa.
Hata hivyo mwanadada huyo hakueleza wazi kama ni lini wanaanza mchakato wakuifanya ngoma yake mpya.
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.