Breaking News
recent

Chege aeleza sababu za kufunga "Chigunda Classic Wear" na "Chigunda Barbershop"

Msanii ambaye anaunda kundi la TMK wanaume family maarufu kama Chege au mwenyewe hupenda kujiita Chege Chigunda mtoto wa mama Saidi, aliwahi kujihusisha na biashara nyingine ya kuuza nguo kwenye duka lake la Chigunda Classic. Duka la Chigunda Classic lilikuwa maeneo ya Kinondoni ndani yake kulikuwa na nguo tofauti. Baada ya kufanya biashara hiyo kwa muda kadhaa, Chege aliamua kulifunga. Baada ya hapo alifungua barbershop ambayo likuwa mitaa ya Kinondoni hapo hapo pia. Lakini muda ulifika akaifunga hiyo barbershop kama ilivyokuwa kwa duka la nguo.


Chege akiongea na chombo cha habari fulani alifunguka kuhusu sababu za msingi zilizomfanya kufunga biashara zote mbili wakati wasanii wengi wanashauriwa kuwekeza pesa zao kwenye biashara nyingine na wasitegemee muziki tu. ”Unajua biashara ni wewe mwenyewe, biashara ni wewe kwa maana ya kwamba unajua uchungu wa pesa uliyoweka hapo kwenye biashara husika na unafahamu malengo yako baada ya muda flani ufike sehemu gani. Sasa mimi ni mtu wa kuzunguka labda kwenye show au vitu vingine vinavyohusiana na kazi yangu. Watu ninaowaacha kwenye hizi biashara walikuwa sio sahihi kabisa. Najikuta napiga hatua mbili mbele harafu tano nyuma. Kitu ambachi kinaniumiza mimi. Hiyo ndiyo sababu ya kufunga duka na barbershop, sikuwa na usimamizi wa uhakika has akwa watu niliokuwa nawaachia hizi biashara

Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.