Breaking News
recent

Genevieve Nnaji ndiye Msanii wa kike Tajiri zaidi Nchini Nigeria

Orodha ambayo inaonyesha wasanii wa kike wa filamu 15 ambao wana vipato vya juu kabisa imetoka ikiwa pia inaonyesha kiasi cha pesa ambacho wanadada hawa hujitengenezea, huku nafasi ya kwanza ikiwa inashikiliwa na bibie Genevieve Nnaji.
Genevieve anafuatiwa kwa karibu sana na Ini Edo, Patience Ozokwo, Omotola Jalade, Kate Heshaw, Stella Damascus, Joke Silver, Ngozi Ezeonu na Rita Dominic, ni kati ya wale mastaa ambao kumuweka katika picha yako, utatakiwa kumlipa zaidi ya Naira Milioni 1, zaidi ya shilingi milioni 10 za Tanzania.
Wengine katika orodha hiyo wamo Chioma Chukwuka, Oge Okoye, Funke Akindele, Mercy Johnson, Fathia Balogun na Uche Jumbo ambapo ni katika kundi la mastaa mbao dau lao halishuki chini ya Naira laki 4 na nusu, zaidi ya shilingi milioni 4 na laki 6 za Tanzania.

Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.