Breaking News
recent

Pancho kufanya kazi na Camp Mulla na Octopizzo

Ni moja kati ya ma producer wakali hapa Tzee wanaotamba kwa kugonga ngoma kali ambazo zinafanya mpaka dzain raia wa hapa bongo land wanasema duuuh!!!!!! kweli huyu producer ni noma najua wajua namzungumzia nani huyu si mwingine anajulikana kwa jina Pancho Latino kutoka  Label ya B hits kwa mtu mzima Hammer B.Habari ambayo tumeipata hivi sasa kwamba producer huyu anatarajia kufanya kazi na wasanii ambao kiukweli kwa sasa  dzain ndiyo wana hits na ngoma zao kali kadhaa kule pande za 254 hawa si wengine nawazungumzia Camp mulla na Octopizzo.Producer huyu anatiririka kama ifuatavyo kuhusiana na habari ambayo tumeipata kwamba anatarajia kufanya kazi na Camp mulla na octopizzo huyu hapa" Yap ni kweli natarajia kufanya nao kazi za muziki kwani kwa sasa ndiyo tupo katika michakato ya mazungumzo kwa hiyo napenda kuwambia wale mashabiki wangu wakae tayari kwa kusikia kile ambacho nitakacho wafanyia Camp mulla na Octopizzo"Hayo ndiyo maneno ya mtu mzima Pancho Latino akifunguka kuhusiana na Camp mulla na Octopizzo kama unavyoona amesema kwamba ndiyo dzain wapo katika mazungumzo ya kuweza kufanya nao kazi kwa hiyo basi tunamtakia mafanikio mema na kazi nzuri atakayo ifanya wasanii hao.
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.