Breaking News
recent

Mwanafunzi wa kike wa chuo kikuu Nairobi aambukiza UKIMWI wanaume 322

Mara zote tangu nianze kulisikiliza tangazo la "TUKO WANGAPI" na kuliona kwenye luninga, nimekua nikisisimuka na hasa kuchukua dakika kadhaa kujiuliza hivi kweli tuko wangapi?.
Jana katika kumalizia weekend yangu, nilikuwa na washkaji maeneo tukipiga soga, na bila kujua tukafikia maongezi yaliyokuwa yanawahusu wadada zetu wanaokaa mabarabarani kwa minajili ya kujiuza, stori ziliendelea na mwisho wake kila mmoja alibaki kimya huku akionyesha kuwaza maisha haya tuliyonayo kwa sasa.

tukiachana na hayo ambayo tunauwezo wa kuyaepuka kwa kuwa muaminifu, hii habari ndio imenifanya kuandika hiki niachokiandika

zimepita takribani wiki nne tangu mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi alipojitangaza kuwa ni HIV positive na aliapa kuwa lazima ausambaze kwa watu kwasababu aliupata ama aliambukizwa wakati alipofanya tendo la ndoa kwa mara ya kwanza

"nimeshalala na wanaume 322 katika campus yangu na wawili kutoka nje.Nilitaka kuwaambukiza watu 2,500 lakini dhamira yangu inanisuta na inaniumiza moyoni".alisema mschana huyo
cha kusikitisha zaidi report hii imekuja miezi miwili tu baada ya msichana mwingine mwanafunzi wa chuo kikuu cha Moi kutoa list ya ya wanaume 90 na kuzibandika kweye notice board akidai amewaambukiza wote virusi na katika list hiyo kulikua na majina mawili ya wanasiasa maarufu nchini Kenya.

msicha huyo amekua na uchungu hata kufikia uamuzi huo wa kuwaambukiza wanaume 322 kwasababu aliambukizwa ugonjwa huo katika siku yake ya kwanza ya kungonoka.
swali nililobaki nalo hapa ni TUNAELEKEA WAPI? VIPI HALI YA VYUO VYETU HAPA BONGO?
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.