Ndugu Waandishi,
Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi
nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti
wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya
uzushi mwingine wowote zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi
cha kuukanganya umma.
Nafahamu
nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima
imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi
wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa,
jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu
kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale
wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania
wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa
taifa.
No comments:
Post a Comment