Breaking News
recent

Hizi ndizo zasemekana kuwa sababu za ugomvi kati ya Peter na Paul wa P Square

Mengi yamezungumzwa juu ya kinachodaiwa kutengana kwa kundi maarufu Africa kutoka Nigeria "PSquare" huku wengine wakidai kuwa ni kutokuelewana kwa Petter na kaka yao mkubwa ambae ndio manager wao "Jude Okoye" huku wengine wakitupa lawama kwa mke wa Petter "Lola" kuwa ndio chanzo maana hata mama yao alipokuwa hai hakupenda Petter amuoe mwanamke huyo ambae licha ya kuwa amemuoa baada ya mama yake kufariki, Kaka yake "Jude" hakuhudhuria harusi yao pamoja na kuwa alikuwepo nchini Nigeria
Leo hii kupitia mtandao wa onlinenigeria umethibitisha sababu za ugomvi mkubwa uliotokea kati ya kaka hao ndugu ambao ni mapacha.
Inasemeka kuwa ugomvi huo ulianzishwa na wasaidizi wao(Personal Asisstants). Msaidizi wa Jude alimpa pesa msaidizi wa Petter akamsajilie gari lake, lakini msaidizi wa Petter hakufanya hivyo badala yake akatumia pesa hizo kwa matumizi mengine.(na ndio kijana alieripotiwa kula pesa zilizokuwa zikanunue  gari la marehem mama yao alipokuwa hai)
habari ikaendelea kuwa msaidizi wa Jude akakasirika sana baada ya kuona pesa zake hakuna na gari lake halijasajiliwa ndio akaamua kumfata msaidizi wa Petter aliekuwa nyumbani kwa kina Psquare (Squareville) , alipofika wakaanza malumbano na kufikia ugomvi mkubwa baina yao, mpaka kufikia kutoana damu, ugomvi ukawa mkubwa kiasi kwamba Petter akaingilia ugomvi na kutaka kumpiga msaidizi wa Jude ndipo Paul nae akaingilia na kumshika mkono kaka yake kwa ajili ya kumzuia.
katika stage hiyo ya ugomvi Petter alizungusha mkono wake na kumpa kitu, inauma Paul mpaka akaanguka chini .Inasemekana Paul hakumrudishia ngumi ila kaka yao mkubwa "Tony" aliingilia  na kuanza kumpiga Petter.
Kwa kile kinachodaiwa na chanzo hicho cha habari ni kuwa Petter anataka kuwa in-charge wa pesa zao, kaka yao mkubwa na manager wao Jude siku zote amekuwa akisimamaia swala hilo huku Paul akitaka iendelee kuwa hivyo hivyo.
ishu ilikuwa imefikia pabaya mpaka kuamua kumleta wakili kwa ajili ya kugawana mali zao, lakini mwisho wa siku hakuna aliesema hiki na cha yule na hiki ni changu na wakili kushindwa kuendelea.

Tweet ya kaka yao "Jude" na Manager iliwashtua sana mashabiki wa PSquare duniani baada ya kuandika "after ten years am done"
lakini Paul amevunja ukimya kwa kuandika katika ukurasa wake wa facebook,

"After the storm comes the calm, hoping for better days ahead as one familly.Gods intervention"
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.