Breaking News
recent

Chidi Benz ashikiliwa na polisi baada ya kumjeruhi vibaya Ex girlfriend, afikishwa mahakamani

Msanii wa Hiphop anaeiwakilisha Ilala, Chidi Benz anadaiwa kushikiliwa na polisi mwishoni mwa wiki baada ya kumpiga na kumjeruhi vibaya mwanadada anaejulikana kama Mwanaisha  ambae anadaiwa kuwa ni mpenzi wake wa zamani.
Kwa mujibu wa Chidi Benz amesema yeye alikuwa akipita nje ya bar iliyo karibu na kwake ilala Flat alipokuwa akirudi nyumbani kwake akiambatana na mpenzi wake wa sasa ndipo aliposkia sauti ikimuita na kumuuliza zaidi ya mara tatu 

" chidi naona uko na mama watoto" kusogea karibu akakuta ni Mwanaisha na wenzake, ndio akamwambia mbona unanichora au kwasababu nipo na dem mkali kuliko wewe unaona wivu, kilichofata ni chupa ambayo Mwanaisha aliirusha ikampata kichwani na kumpasua damu zikatoka ndipo yeye alimshika nywele Mwanaisha na baada ya hapo kilichofata hakumbuki maana alikuwa amelewa.
Chidi Benz anashikiliwa na polisi na leo hii kesi imeenda mahakamani ambapo hakimu ameamuru kuendelea kushikiliwa kwa Chidi baada ya hali ya mwanaisha kuwa mbaya kiasi cha kushindwa kuongea.
Mwanaisha ameshonwa nyuzi 18 mdomoni, uso umeumuka na kichwa kimemvimba sana.
Mwanaisha mwenyewe huyu hapa akiwa hospitali
 
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.