Breaking News
recent

M-Rap atoa tamko lake kwa Pancho Latino

Msanii wa Kufoka foka hapa Bongo Richard Alibalio aka M Rap wiki kadhaa zlizopita ali-make headline kwenye mdeia za hapa Tanzania kutokana kuibuka ugomvi kati yake na aliyekuwa msimamizi wa kazi zake na ndiye producer wa BHits Pacho Latino.


M Rap kwa sasa ana ngoma moja mpya inafahamika kwa jina la ‘Usiende Mbali’ aliyomshirikisha Jux aliufanya kwenye studio ya AM Records producer ni Maneck baada ya kutoka BHits right now MRap ametoa kauli yake ya mwisho kwa mabosi wake wa mwanzo.
“Nashukuru Mungu nimeishi vizuri na watu nilikuwa nafanya nao kazi kama Vanesa, Jux na wote tuliokuwanao lebo moja, mimi moyo wangu upo safi kabisa na nashukuru coz nimejifunza mambo mengi na kila kitu huwa kinatokea kwa sababu.
Alisema “Kwa sasa nipo chini ya Maneck ambapo nilipokuwepo mwanzo kabla B hit hawajaniona na wala sikuondoka kwa ugomvi so nimerudi wamenipokea kwa mikono salama na kwa sasa siko tayari kwenda mahali pengine bila kuwa na uhakika wa kufanya kazi na watu serious.”
Alimalizia kwa kusema “Kiukweli ni ngumu sana kufanya kazi na mtu ambaye hautakuwa na uhuru na anayejiona muhimu kuliko wewe wakati tunaishi kwa kutegemeana, asante kwa mashabiki wangu ambao bado wapo na mimi bega kwa bega so wategemee mambo mazuri kutoka kwangu.”
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.