Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na
Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika
wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Gerald ambaye
alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana
hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa
mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24.
Wawili hao bado
wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.
Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi
sasa ni janga la kitaifa nchini.
Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika
nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya
nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na
masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
No comments:
Post a Comment