Breaking News
recent

Zitto Kabwe: 2015 sitagombea ubunge

Baada ya kusikia kupitia  vyombo mbali mbali vya habari kuwa Mh mbunge wa Kigoma Mjini Zitto ametangaza kuwania kiti cha uraisi ifikapo mwaka 2015, Zitto ameendelea kusisitiza msimamo wake kupitia mtandao wa jamii wa Facebook
Narudia, mwaka 2015 sitagombea Ubunge. Nitafanya kampeni ya Urais, ama mimi kama mgombea wa chama changu CHADEMA au kama mpiga debe wa mgombea wa chama changu. Miaka 10 ya Ubunge inatosha na kwa ngazi hiyo ni vema niwaachie wengine wasukume mbele gurudumu la maendeleo ya Jimbo na mkoa wetu. Huu ndio uamuzi wangu wa mwisho na nimeshawaeleza wananchi wa Jimbo langu na mkoa wa Kigoma toka mwaka 2005
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.