Breaking News
recent

Samatta apata leseni Belgium na kununua ndinga ya Millioni 130

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya KRC Genk ya ligi kuu ya Belgium – Jupiter League – Mbwana Ally Samatta, jana kupitia akaunti ya Instagram ameonyesha ‘ndinga’ yake aliyoinunua baada ya kupata leseni ya kuendesha gari nchini Belgium.

Samatta ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa baada ya kupata majeruhi, jana usiku alikuwemo katika katika kikosi cha Genk kilichoifunga Sassuolo 3-1 katika mchezo wa Europa League.

Gari alionunua Samatta ni Merecedez Benz Cla220 Cdi AMG Sport 2016 – ambayo imemgharimu kiasi cha €46,680 ambayo ukiizidisha kwa fedha za madafu inakuwa zadi ya millioni 130.
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.