Breaking News
recent

Jina la Wimbo mpya wa Ommy Dimpoz na Maana yake Halisi viko hapa.

Utafahamu kuwa miezi miwili nyuma kuna wimbo ulivuja kutoka kwenye maktaba ya Ommy Dimpoz na baada ya saa chache alitoa ombi kwa vyombo vya habari kutocheza wimbo huu kwani haukuwa kwenye mpango wa kutoka muda ule.

Kwenye Exclusive Interview  na  chombo flani cha habari, Msanii Ommy Dimpoz  amesema ni miezi nane sasa hajatoa wimbo toka Tupogo itoke na ni muda mrefu kukaa kimya, kabla ya mwisho wa mwezi wa Nne anampango wa kutoa wimbo mpya utaoitwa “Ndagushima”.
“Ndagushima” ni neno la lugha ya Kiha inayotumiwa zaidi Kigoma na Linex ndiye amemsaidia kupata wazo hilo. “Ndagushima” maana yake ni “Nakupenda Sana” au ” I'm in love With You”. Ni Neno linalotumika kama unataka kuonyesha mapenzi mazito na ya ukweli zaidi.
Dimpoz amethibitisha Kuwa wimbo unatoka ndani ya mwezi wa nne na video alifanya Uingereza nayo inatoka.
Kuhusu kuchelewa kwa video ya Tupogo, Dimpoz amesema anapishana muda wa kazi na J Martins ndio maana mpaka leo hawaja shoot video ya hit song Tupogo.
Mohamed Jaku

Mohamed Jaku

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.